HAYA NI MAMBO SABA (7) AMBAYO WANAUME WENGI HAWAYAPENDI:
*1.MWANAMUME HAPENDI KUFOKEWA:*
🍃🎒▫️ Hata Kama amekosea; jaribu kumuonyesha kosa lake pasipo kumfokea au kumvunjia heshima.
*2. MWANAMUME HAPENDI KUULIZWA MASWALI MENGI KWA WAKATI MMOJA:*
🍃🎒▫️ Ukimuuliza swali halafu yeye anakua kimya au anaduwaa; ujue hana jibu au anajisikia vibaya kuhusu jibu ambalo anatakiwa kutoa. Mpe muda ajipange kutoa jibu usimlazimishe siyo mtumwa wako.
*3. MWANAMUME ANAHITAJI MUDA WA KUKAA KIMYA; USIMLAZIMISHE KUONGEA:*
🍃🎒▫️ Zaidi sana anapopita kwenye hali ngumu au changamoto fulani; wanaume wengi hupenda kukaa kimya huku akiwaza nini cha kufanya.
🍃🎒▫️Tofauti na wanawake, ambao wakati wa changamoto ndipo wanataka kuongea zaidi.
🍃🎒▫️ Wanaume wengi hawapendi kuongea kama hawana suluhisho la shida iliyopo mbele yao hivyo Kama wewe ni mtu sahihi kwake jifunze kumsoma mumeo ili ujue nyakati zake ngumu ili usimame kwenye zamu yako.
*4. MWANAMUME HAPENDI MKE MWENYE KIHERE-HERE:*
🍃🎒▫️Yani hata kama bado hajakwambia, kaa ukijua kwamba wanaume hawapendi kuwa na mke ambaye hapitwi na jambo.
🍃🎒▫️ Mwanamke anayetaka kuchangia kila kitu au kuongea-ongea sanaaaa! Mmmhhh! Unamchosha mwanamumeo.
*5. MWANAMUME HAPENDI MKE WAKE AWE NA MARAFIKI WEEENGIII;*
🍃🎒▫️hivyo mwanamume hapendi kuona mke wake yuko bize “ku-entertain” watu wengine *(HATA KAMA HAKUNA MAHUSIANO MABAYA).* Mara huyu ni rafiki yangu tulisoma nae, niliwahi fanya nae training, ni mwalimu wa kwaya, oohh huyu tulifanya nae kazi, bla, bla , bla zako zitakuvunjia mji tumia akili ipasavyo.
*6. MWANAMUME HAPENDI KUNYANYASIKA:*
🍃🎒▫️ Wanaume wengi ni rahisi kusumbuliwa na hali au hisia ya kujiona duni (Inferiority Complex).
🍃🎒▫️Zaidi sana kama MKE ndiye mwenye pato kubwa, au elimu kubwa, umri mkubwa, au anatoka familia yenye nguvu zaidi kuliko ya mume. ( Lakini ni kwa hasiyejiheshimu) 🍃🎒▫️Hapo inabidi mwanamke awe makini sana maana kitu kidogo tu kinaweza sababisha mwanaume adhanie kwamba tayari anadharaulika. Mwanamke anahitaji *HEKIMA* ya juu kuishi na mume mwenye shida ya kujidharau.(Faida ya *MKE MWENYE HEKIMA* inatenda kazi Sana mahali hapa)
7 MWANAMUME, HAPENDI KUPOTEZA MAMLAKA AU SAUTI YAKE KWA MKE WAKE:*
Mwanamume akiona dalili za kupoteza mamlaka yake na kukosa sauti kwa mkewe, basi hujaribiwa kutafuta mahali pengine pa kuonyesha hiyo mamlaka.
*🍃🎒▫️Ni rahisi KUMPENDA* Mke mwenye *UTII;* Vilevile, ni rahisi *KUMTII* Mume mwenye *UPENDO*
🍃🎒▫️“Kila MWANAMKE* aliye na *HEKIMA* *HUJENGA* nyumba yake; Bali aliye *MPUMBAVU HUIBOMOA* *NYUMBA YAKE* kwa mikono yake *MWENYEWE*
🍃🎒➿➿➿➿➿➿➿➿🎒🍃
0 Comments